Job 20:19-23


19 aKwa kuwa aliwaonea maskini na kuwaacha pasipo kitu;
amenyang’anya kwa nguvu nyumba asizozijenga.


20 b“Hakika hatakuwa na raha katika kutamani kwake sana;
hawezi kujiokoa mwenyewe kwa hazina zake.

21 cHakuna chochote kitakachosalia kwa ajili yake ili ale;
kufanikiwa kwake hakutadumu.

22 dKatikati ya wingi wa ustawi wake, dhiki itampata;
taabu itamjia kwa nguvu zote.

23 eAtakapokuwa amelijaza tumbo lake,
Mungu ataionyesha ghadhabu kali dhidi yake,
na kumnyeshea mapigo juu yake.
Copyright information for SwhKC